Nauli ya Treni SGR Dar to Dodoma. Safari ya treni ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kupitia Reli ya Kisasa ya Standard Gauge Railway (SGR) ni mojawapo ya maendeleo makubwa katika sekta ya usafiri nchini Tanzania. Huduma hii inatoa njia salama, haraka, na ya kisasa kwa abiria wanaosafiri kati ya miji hii miwili mikubwa. Katika makala hii, tutajadili kwa undani kuhusu nauli ya treni SGR Dar to Dodoma, ratiba, na huduma zinazopatikana.
Nauli ya Treni SGR Dar to Dodoma
Kwa mujibu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), nauli za treni ya kawaida kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma (kilomita 444) ni Tsh 31,000 kwa abiria mzima. Kwa watoto wenye umri wa miaka 4 hadi 12, nauli ni nusu ya bei ya mzima, yaani Tsh 15,500. Watoto chini ya miaka 4 hawatalipia nauli. Na Pia Nauli za Treni ya Haraka (Express) kwa daraja la Biashara (Business class) kutoka Dar es salaam hadi Dodoma ni Tsh 70,000 na kwa daraja la Juu (Royal Class) Tsh 120,000.
Vituo vya Kusimama
Treni ya haraka inasimama katika vituo viwili pekee Dodoma Kituo cha mwisho cha safari na Morogoro Kituo cha kwanza cha kusimama, huku Treni ya kawaida inasimama katika vituo vingi, ikiwemo Pugu, Soga, Ruvu, Ngerengere, Morogoro, Mkata, Kilosa, Kidete, Gulwe, Igandu, na Bahi, kabla ya kufika Dodoma.
Mapendekezo ya Mhariri: