Ulishawahi kujiuliza je, Mkuu wako wa mkoa anapokea mshahara wa kiasi gani? katikata makala hii tumeandaa taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vinavyoelezea mada hiyo. Mshahara wa Mkuu wa Mkoa ni miongoni mwa masuala yanayozua mjadala mkubwa nchini Tanzania. Ingawa nafasi hii ni ya heshima na inahusisha majukumu makubwa ya kiutawala na kisiasa, kiwango cha mshahara na marupurupu ya viongozi hawa hakijatangazwa rasmi na serikali. Hii imekuwa chanzo cha uvumi na mjadala miongoni mwa wananchi na wadau wa utawala bora.
Majukumu ya Mkuu wa Mkoa
Mkuu wa Mkoa anateuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ana jukumu la kuratibu na kusimamia utekelezaji wa sera za serikali katika mkoa wake. Majukumu yake ni pamoja na:
- Kusimamia utawala bora na maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika mkoa.
- Kuratibu shughuli za serikali za mitaa na kuhakikisha zinazingatia sera za kitaifa.
- Kuwa kiungo kati ya serikali kuu na serikali za mitaa.
Mshahara na Marupurupu ya Mkuu wa Mkoa
Kwa mujibu wa taarifa zisizo rasmi, baadhi ya vyanzo vinadai kuwa:
- Mshahara wa msingi: Tsh milioni 5.5 kwa mwezi
- Posho na marupurupu: Hadi Tsh milioni 14 kwa mwezi, ikiwa ni pamoja na posho za vikao, nyumba, usafiri, na kiinua mgongo cha mara kwa mara.
Hata hivyo, taarifa hizi hazijathibitishwa rasmi na serikali, na kuna tofauti za maoni kuhusu kiwango halisi cha malipo haya.