Orodha ya Majina ya walioitwa usaili air Tanzania. Kampuni ya Ndege Tanzania kinapenda kuwataarifu wote walioomba kazi katika kada mbalimbali
kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa kuanzia jumamosi, tarehe 3 Mei, 2025.
Wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-
- Usaili utafanyika Jumamosi, tarehe 3 Mei, 2025 saa moja na nusu asubuhi kama
ilivyooneshwa kwenye tangazo hili; - Muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada;
- Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;
- Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkaazi, Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha kazi, Kitambulisho cha Taifa, Hati ya Kusafiria au Leseni ya udereva;
- Wasailiwa wanatakiwa kufika na vyeti vyao halisi, kuanzia cheti cha Kuzaliwa, Kidato cha IV, VI, Astashahada, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji;
- Wasailiwa watakaowasilisha “Testimonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati za matokeo za Kidato cha IV na VI (Form IV and Form VI result slips) HAZITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI
- Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi;
- Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili;
- Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakukidhi vigezo
- Wasailiwa wenye tofauti ya majina katika vyeti vya elimu, taaluma na cheti cha kuzaliwa wahakikishe wanakuwa na kiapo cha kubadilisha majina kilichosajiliwa (DEED POLL);
- Wasailiwa waliozaliwa nje ya Tanzania wahakikishe wanawasilisha uthibitisho wa uraia kutoka Ofisi uhamiaji
BONYEZA HAPA KUDOWNLOAD MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI AIR TANZANIA
Mapendekezo ya Mhariri: